Thursday, May 30, 2013

Juhudi za wabunge wa Kenya kuongezewa mshahara zaingia doa


Mahakama nchini Kenya

imesimamisha utekelezaji wa

nyongeza ya mishahara ambayo

wabunge wa nchi hiyo

walipendekeza kujiwekea. Chama

cha mawakili nchini Kenya

kiliwasilisha ombi la kutaka

kuwekewa amri ya kisheria wabunge

hao siku moja baada ya wabunge

hao kupiga kura ya pamoja kutaka

wajoingezee mishahara.

Wanaharakati wamekuwa wakipinga

jaribio hilo huku wakiandaa

maandamano katika barabara za jiji

la Nairobi wakimuomba rais

asiidhinishe kura hiyo.

Hapo jana Rais Uhuru Kenyatta

aliwafokea wabunge hao kwa uamuzi

wao huku akisema kuwa mishahara

ya wafanyikazi wote wa Umma

inadhibitiwa na tume ya mishahara

iliyoundwa.

Kwa upande wao wabunge hao

wameishutumu tume hiyo wakidai

kuwa ilivuka mpaka wake

kupendekeza wapunguziwe

mishahara yao kwa takriban asili

mia hamsini kutoka dola elfu kumi

kwa mwezi.

Wabunge hao wameelezea hasira

zao juu ya tamko la Rais Uhuru

Kenyatta na tume ya kudhibiti

mishahara ya maafisa wa serikali

ambao wanasema waache vitimbi

vyao vya kutaka kuongezwa

mishahara.

Wanatishia kubadilisha sheria ya

idadi ya maafisa wanaoweza

kuhudumu katika tume za serikali

hadi watatu , kupunguza mishahara

ya maafisa wa serikali kwa asilimia

hamsini na saba na kuwaondolea

wananchi wanaopata chini ya

shilingi elfu hamsini kama ajira

uwezo wa kutozwa kodi.

Wabunge hao hata hivyo hawaoni

ubaya wowote wa kulalamika kuwa

mishahara yao inapunguzwa

wakisema wanasubiri tume ya

bunge kuwalipa mishahara yao ya

laki nane na hamsini kutoka laki

tano

Location : Kisinane Rd, Moshi,
Poudly supported by washari company

No comments:

Post a Comment