Thursday, May 23, 2013

Mjue peter tosh



Peter Tosh (19 Oktoba

1944 – 11 Septemba 1987)

huyu alikuwa ni

mwanamuziki Mjamaika wa

mtindo wa rege, alikuwa

na kipaji mahiri cha

kutunga mashairi ya

muziki, pia alikuwa ni

mpigaji mahiri wa gitaa.

Peter alizaliwa tarehe 19

Oktoba 1944, akiwa ni

mtoto pekee wa mama

Alvera Coke, baba yake

aliitwa James Mclntosh

ambaye alikuwa ni

mhubiri wa kanisa la

Savanna-la-mar. Peter ni

jina ambalo alibadilisha

lakini jina lake halisi ni

Winston Hubert Mclntosh.

Katika maisha yake

hakubahatika kulelewa na

baba na mama yake,

alilelewa na shangazi yake

sababu wazazi wake

hawakuwa na muda wa

kumlea, hivyo huwezi

kuamini alijitunza

mwenyewe kwa baadhi ya

mambo bila kupata

matunzo kutoka kwa baba

yake ambaye alikuwa ni

baba wa watoto wengi.

Peter alianza kupiga ala

za muziki akiwa kijana wa

umri mdogo, alijifunza

kupiga kinanda kwa miezi

sita pia alijifunza kupiga

gitaa, ala hiyo ndiyo iliyo

kuja kumpa umaarufu,

mwaka 1956 baada ya

kuondoka Savanna-la-mar

Peter na shangazi yake

walikwenda mji wa

Denham katika jiji la

Kingston, Peter alipofikia

umri wa miaka kumi na

tano shangazi yake

alifariki, hivyo alikwenda

kwa mjomba wake West

Road huko Trench Town.

Peter alikutana na Robert

Nesta Marley (Bob Marley)

na Neville O'Reilly

Livingston (Bunny Wailer)

na wakajiunda kuwa

watatu wa kwanza wa

Wailer halisi na wakajiita

Wailin'Wailers, na

walianza kuimba pamoja

mwaka 1962 na alikuwa ni

yeye tu kati yao aliyeweza

kupiga ala, hivyo alifanya

bidii ya kuwafundisha

wenzake na alikuwa ni

mmojawapo

aliyemfundisha Bob

kupiga gitaa. Peter alijitoa

Wailers mwaka 1974 hii ni

baada ya Chris Blackwell

kukataa kutoa albamu yake

ya kwanza yeye akiongoza

safu ya uimbaji.

Location : Kisinane Rd, Moshi,
Posted via Blogaway

No comments:

Post a Comment