Thursday, May 30, 2013

Mchungaji afedheheswa baada ya kufumaniwa live na mwanakwaya



Habari zilizoripotiwa na mtandao wa

Kenyan-Post zinasema msichana

huyo mweye miaka 23 amekuwa na

mahusiano ya muda mrefu na pasta

huyo kabla hawajabambwa.

Kisa hiki ni kama movie ambazo

tumezoea kuziona zenye story line

ambayo unaweza kutabiri mwisho

wake.

Kwa mujibu wa mtandao huo, ile

‘siku ya 40’ mke wa pasta huyo

alikuwa anatarajia kusafiri kwenda

nyumbani kwao kusalimia wazazi

wake hivyo mumewe alimsindikiza

mpaka kituo cha basi, lakini

alionekana kuwa mtu mwenye haraka

na kumwambia mkewe kuwa siku

hiyo ana mkutano muhimu hivyo

anapaswa kuwahi. Baada ya

kumfikisha kituoni aligeuza gari kwa

haraka na kuondoka.

Huku nyuma mke wa pasta kwa

bahati mbaya (upande wa pasta) na

bahati nzuri (upande wake)

aligundua kuwa amesahau zawadi

aliyokuwa amemnunulia mama yake

mzazi ambaye ndio anaenda

kumsalimia hivyo ikabidi airudie

nyumbani kisha asafiri na basi

litakalokuwa linafuata.

Alipofika nyumbani anapoishi na

mumewe alishangaa kukuta mlango

haujafungwa kwa nje na huku

anakumbuka walipoondoka

waliufunga hivyo akahisi huenda

wamevamiwa mchana kweupe,

alipojaribu kuusukuma ulikuwa

umefungwa kwa ndani ndipo

alipoomba msaada wa majirani

wakavunja kitasa na kuingia ndani.

Mama huyo alipigwa na butwaa kwa

kile alichokikuta ndani baada ya

kumkuta msichana anayemfahamu

kuwa kiongozi wa kwaya ya kanisani

la mumewe wakiwa uchi wa mnyama

katika kitanda chake na mumewe.

Maamuzi aliyochukua ni kuwavamia

kitandani na kuzitupa nje kupitia

dirishani nguo zao wote lakini kwa

bahati mbaya msichana

aliyemfumania alifanikiwa kukimbia

na kumuacha pasta mwenyewe.

Huwa wanasema hasira ni hasara na

maamuzi ya hasira hugeuka majuto

baadae, baada ya mmbaya wake

kukimbia aliamua kumvuta mumewe

(pasta) akisaidiwa na watu

wengine akiwa uchi wa mnyama na

kumtembeza mbele ya umati wa

watu mpaka katika kanisa analotoa

huduma pasta huyo kwa lengo la

kufichua mabaya yake.

Bahati nzuri alijitokeza mwanaume

mmoja aliempatia shati lake ili

ajisitiri.

0

Location : Lema Rd, Moshi,
Posted via Blogaway

No comments:

Post a Comment