Tuesday, May 21, 2013
Kikwete amwagia sifa lowassa
Rais Jakaya Kikwete
amemwagia sifa Waziri Mkuu
wa zamani, Edward Lowassa
hatua ambayo inaweza
kutafsiri mengi katika
medani ya siasa nchini.
Akizungumza na wabunge wa
CCM kwenye Ukumbi wa White
House Dodoma juzi, Rais
Kikwete ambaye pia
mwenyekiti wa chama hicho,
alisema nguvu za Lowassa
pekee zinatosha kushinda
uchaguzi mdogo wa kiti cha
udiwani Kata ya Makuyuni
kilichoko wilayani
Monduli.
Kata ya Makuyuni iko
wilayani Monduli, ambako
Lowassa amekuwa mbunge
wake tangu mwaka 1995.
Habari za kutoka ndani ya
kikao hicho zinaeleza kuwa
Rais Kikwete alitoa kauli
hiyo kuhusu kampeni za
uchaguzi huo wa Makuyuni,
baada ya kuwa ametoa ruksa
kwa makada wa chama hicho
wanaotaka urais kuanza
kujipitisha pitisha
miongoni mwa wanachama wa
chama hicho. Lowassa
anatajwa kuwa miongoni mwa
wanaCCM wanaotaka kumrithi
Rais Kikwete kwenye
Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
“Sina tatizo na pale
Makuyuni, najua muscles
(misuli) za Mzee Lowassa
zinatosha kutupa ushindi;
au vipi mzee?” alidokeza
mmoja wa wabunge wa CCM
akimnukuu Rais Kikwete.
Uchaguzi wa Udiwani Kata
ya Makuyuni unaotarajiwa
kufanyika Juni 16, mwaka
huu, utakuwa wa ushindani
mkali kati ya CCM na
Chadema ambao historia yao
kisiasa mkoani Arusha ni
ya uhasama.
Katika uchaguzi huo,
unaofanyika baada ya kifo
cha Abdillah Warsama
(CCM), chama hicho
kitatetea nafasi yake kwa
kumsimamisha Godluck
Lerunya na Chadema ni
Japhet Sironga. Mbali na
Kata ya Makuyuni, uchaguzi
wa udiwani mkoani Arusha
utafanyika pia katika Kata
za Kaloleni, Themi,
Kimandolu na Elerai,
kutokana na waliokuwa
madiwani wa kata hizo
(Chadema), kufukuzwa na
chama chao.
“Mnaweza kuchafuana leo,
kesho mkapata mgombea
mwenye nundu nyingi na
mabandeji kila mahala,
halafu mkapata shida
kumnadi,” alisema.
Siyo mara ya kwanza kwa
Kikwete kumsifia Lowassa
kwani aliwahi kufanya
hivyo mwaka jana huko
Longido wakati akikabidhi
ng’ombe.
Pia aliwahi kumsifia
wakati wa kampeni za
uchaguzi za mwaka 2010
wakati Kikwete
alipomwelezea Lowassa kama
Mbunge makini na kuwaomba
watu wa Monduli kumchagua
tena.
Hata hivyo, alipoulizwa
kama baada ya kuruhusiwa
kuanza kujipitisha kwa
wanaCCM kama anataka
kuwania urais, Lowassa
alijibu kupitia watu wake
wa karibuni kuwa
asingependa kuzungumzia
suala hilo hasa baada ya
Rais kutoa kauli hiyo.
Kutangaza nia ruksa
Rais Kikwete aliwaeleza
wabunge hao kuwa si kosa
kwa watu kutangaza nia ya
kugombea nafasi mbalimbali
za uongozi ikiwamo urais
mwaka 2015.
“Wabunge na mawaziri wenye
nia ya kutangaza nia ya
kugombea urais wawe huru,
kwani hiyo ni haki yao,
isipokuwa wafanye kwa wema
bila kukivuruga chama na
kuwagawa wanaCCM katika
makundi. Sioni tatizo watu
kujipitisha. Sisi sote
hapa tulijipitisha. Lakini
tufanye hivyo kistaarabu
bila kuvurugana.”'
Aliwaagiza wabunge wa
chama hicho kwenda
majimboni mwao kusikiliza
kero za wananchi badala ya
kusubiri wakati wa
uchaguzi.
Membe
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa,
Bernard Membe ambaye naye
anatajwa kuwa miongoni mwa
wagombea amewataka
waandishi waache kuandika
kila siku habari za urais
na badala yake waandike
mambo ya maendeleo.
Akizungumza na waandishi
wa habari jana baada ya
kukutana na mabalozi wa
nchi zinazoendelea kuhusu
Mkutano wa Smart
Partnership, unaotarajiwa
kufanyika nchini, Membe
alisema ni vizuri
yakaandikwa mambo ya
maendeleo na si kila
wakati kuandika mambo ya
urais.
“Mkutano kama huu nchi
kama Kenya watauripoti
vizuri na kwa undani hivyo
mfanye hivyo si kila kitu
urais 2015,” alisema
Membe. Mkutano huo utaanza
Mei 28, hadi Juni Mosi na
utajadili jinsi gani
sayansi na teknolojia
vinaweza kutumika
kuzikwamua kiuchumi. wa kitaa
Location : Lema Rd, Moshi,
Posted via Blogaway
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment