Sunday, May 19, 2013

Waraka wa vinega huu hapa



Ni wazi na dhahiri kabisa kesi

iliofunguliwa mahakamani dhidi ya

Lady JayDee haina maana yoyote

isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa

muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa

kuwa waraka wa piliulikuwa utoke tar

15 may na mwingine tar 17 may

mwaka huu wa 2013.

Hapa la kujiuliza ni juu ya interview

ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti

suala limefika mahakamani,kweli

Kusaga na Ruge mmeweza

kuthibitisha nyie ni mafisadi na

mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye

nina uhakika anajua kuwa nyie ndio

kikwazo kikubwa na hata Bungeni

alishawahi kuzungumza kuwa alitoa

studio na pango kumbe tatizo sio

hilo,tujiulize wote kuna nini

wanachoficha hadi kumtafutia kesi

raia mwema asie na hatia?

Tena anaejitafutia rizki ambayo wao

wanapigana nayo kwa

kumkandamiza?

Huku wakitumia mabavu wakilindwa

na baadhi ya viongozi wa serikali na

waandishi ambao majina yao

mtayapata kupitia nyaraka

zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa

kwanza.

Nimesikitika sana na njia pekee ya

kuufahamisha umma juu ya ufisadi

huu wa Ruge Mutahaba na Joseph

Kusaga ni kuyaanika yote ambayo

jamii na Viongozi wa Serikali kama

mlikuwa hamjui sasa ndio wakati

muafaka wa kuwajua watu hawa

ambao kila kukicha ni kuimarisha

ufisadi wao na kujipendekeza kwa

Viongozi sambamba na watoto wao

(mtajua mpaka majina yao)

Naanza kupatwa na wasiwasi

nikijiuliza, endapo Lady JD angekuwa

amegombana na msanii mwenzake

mkubwa kama Prof Jay, Ray C au

Juma Nature wanasiasa wangeingilia

kati? Ni wazi wasingesogea kwa kuwa

hakuna maslahi zaidi ya kuingilia

mgogoro huu ambao hawataki jamii

ijue maovu yao.

Napatwa mashaka jinsi wanasiasa

wanavyolivalia njunga jambo binafsi

Kama hili na kulifanya ni la kiserikali

basi tafuteni chanzo cha tatizo mjue

ni sehemu gani sahihi ya kuanza

kutatua kilichopo na sio kukimbilia

kuunda vikao ambavyo naamini

vimeshaitishwa vingi sana lakini

hakuna kilichosaidia.

Wanasiasa badala ya kutafuta

sababu zinazofanya wasanii

wanalalamika mnakimbilia kutatua

mgogoro wa Ruge na JD ili

kusuluhisha mambo yasiendelee

kuongelewa jamii ijue uovu wa

mafisadi hawa.

Haitasaidia kwa sababu wanaojua

maovu ya hawa mafisadi Rugen na

Kusaga ni wasanii wengi wakubwa na

watu wengine binafsi (kumbukeni

waraka zipo 88)

Vijana mnaowategemea katika

kampeni zenu na mnawaita Taifa la

kesho, lakini mnakubali waendelee

kukandamizwa na kunyanyasika huku

wakizidi kuwaneemesha kina Ruge na

Kusaga.

Tatizo mnalijua kaeni na wasanii

wote wawaelezee matatizo yao,

msikae na wasanii ambao

wanaamrishwa na kina Ruge.

Sikilizeni kilio cha wasanii wengine

pia na itafutwe njia ya kupata maoni

ya kila mmoja na kuachana na watu

wengine ambao wanaendesha

mtandao wa ufisadi chini ya kivuli

cha Ruge (Said Fella na Babu Tale)

ambao mtapata kujua kila kitu

kuhusu ufisadi wao na

kinachoendelea (kumbuka waraka

zipo 88)

Ruge Mutahaba amekuwa ni tatizo

na janga la Kitaifa katika tasnia ya

muziki kwa ujumla, amekuwa

akiwagawa wasanii kwa kutumia

redio Clouds kwa vitisho vya

kutopigiwa nyimbo, au kwa

danganyio la kufanyiwa promotion

mpaka kwenye magazeti endapo tu

utakuwa chini ya bawa lake.

Wasanii wamekuwa hawalipwi vizuri

ili waendelee kumtegemea fisadi

huyu.

Kwani wasanii wote wangekuwa na

kipato cha kuweza kusimama imara

leo hii kauli kama ya Lady JD

ingezungumzwa karibu na kila

mwanabongoflava.

Fred Kavishe (fisadi mwingine)

ambae anasimamia Kili music awards

yuko bega kwa bega na Ruge

kudanganya wananchi nani ni bora

katika tuzo hizo ili kulinda maslahi

yao binafsi.

Na wao huchagua wale wasanii

ambao hawana sauti za kudai haki

yao ili wawatumie kadri

wanavyotaka.Tuzo za Kili ni uozo

mtupu.Imefikia wakati basata itoe

vibali kwa wadau wengine wa muziki

(nako kuna ufisadi)wasio na interest

binafsi na wasanii wao, kuendesha

hizi shughuli ili kukuza

muziki.Kutokuwepo na tuzo zingine

kunasababisha ionekane kuwa

basata nao wamo kwenye mgao wa

mabepari hao wanaoua sanaa ya

Tanzania

Location : Kisinane Rd, Moshi,
Posted via Blogaway

No comments:

Post a Comment