Wednesday, May 29, 2013

Kaka wa coobama kuelekea south Africa



Kaka mkubwa wa

marehemu kusafiri leo

kuufuata mwili wa

Mangwea Africa Kusini

admin May 29th, 2013

0 Comment

Habari zilizopatikana muda huu

zinasema kuwa familia ya Mangwea

inajipanga kutuma ndugu kwenda

Africa Kusini leo (May 29) kwaajili ya

kufanya utaratibu wa kurudi na

mwili wa Marehemu Albert

Mangwea.

Akiongea na Bongo5 muda mfupi

uliopita dada wa marehemu aitwaye

Evelyn, amesema kuwa anahitajika

ndugu wa marehemu asafiri kwenda

Africa Kusini kwaajili ya kufanya

utaratibu wa kurudi na mwili,

sababu kule hawawezi kumtoa na

kumsafirisha bila ndugu yake wa

karibu kwenda.

Kwa Mujibu wa Evelyn familia iko

katika mipango ya mwisho ya safari

hiyo ambayo kaka yao mkubwa na

Mangwea ndiye anayetarajia kusafiri

leo hii (May 29) kwenda South Africa

kuufuata mwili.

“Habari mpya ni kwamba mtu atoke

hapa Tanzania aende akachukue

mwili kule hawawezi kuconfirm yaani

kumtoa kumsafirisha bila ndugu yake

wa karibu kutoka huku, kwahiyo ndio

process zinafanywa, kaka yake

mkubwa ambaye ni kaka yetu atoke

hapa aende South, ndio nadhani

atarudi na huo mwili. Ataondoka leo

hii hii muda wowote na wakati

wowote, “Alisema dada wa

marehemu Albert Mangwea.

Msiba wa rapper kipenzi cha wengi

Ngwea uko Mbezi Beach Goigi kwa

baba yake mdogo , ukishuka goigi

ukiulizia kwa mzee Mangwea kwenye

msiba utaelekezwa. R.I.P

Brother

0

Location : Lema Rd, Moshi,
Posted via Blogaway

No comments:

Post a Comment